Somo LA 1

SOMO LA 1

Ili sentensi yako ya kiingereza iwe sahihi, ni lazima angalau iwe na sehemu 3.

1. Mtendaji wa Kitendo
2. Kitendo
3. Wakati ambao kitendo hufanyika ( tenses)

Tutaanza na Mtendaji.

Kuna watendaji wa aina tofauti, ktk wingi na ktk umoja;

Tuna ;

1. Mimi ...  ...... Sisi
       I/me.......we/us

2. Wewe.............Nyinyi
     You.................You

3.  Yeye..................Wao
      He/ him ......They/ them
      She/ her.  .....They/ them

4. Hicho ( kitu) Huyo ( mnyama). .....It

Hivyo ( vitu) Hao ( wanyama)..... They/ them

Sasa tutachambua hizi sehem 3 ili tuweze kujieleza kwa kiingereza fasaha

Duniani kote lazima kitendo kikitendwa kiwe kimetendwa na mmoja wa hao

Swali ni, kwa nn kwa kiswahili tuwe na jina moja ila kwa kiingereza yawe mawili??

Mfano ;
Mimi( kwa kiswahili). ...I/ me ( kwa kiingereza)
Au ;
He/him ( yeye wa kiume),
She/ her (yeye wa kike)
We/us (sisi)

Tofauti ya I na me ni nini?? Kwa nini tuwe na majina mawili kuwakilisha kitu kile kile?

Fuatilia somo la 2 kujua.

Comments

Popular posts from this blog

Somo LA 2

THE BOOK TO GET NOW !